Powered By Blogger

Sunday, January 20, 2013

Mzee Yussuf kuunguruma Travetine usiku huu

'Big Daddy' Mzee Yussuf

Kiongozi wa Jahazi Mfalme Mzee Yussuf usiku huu atakonga nyoyo za mashabiki wake katika ukumbi wa Travetine Hoteli Magomeni.

Mzee Yussuf akiwa na waimbaji wake wote mahiri watapanda jukwaani katika onyesho lao kabambe litakaloanza saa tatu usiku mpaka majogoo.

Onyesho hilo, Jahazi litapiga nyimbo zake zote zinazotamba na zile zilizotamba ambazo bado zinawika kwenye viunga mbalimbali vya burudani ndani na nje ya nchi.