Powered By Blogger

Sunday, January 20, 2013

Chelsea yairarua Arsenal, mechi bado inaendelea

Frank Lampard

Chelsea imeimarisha nafasi yake ya kusonga mbele kwenye msururu wa ligi kuu ya premier kwa kuilaza Arsenal magoli mawili katika muda 20 ya kipindi cha kwanza ya mechi yao inayoendelea katika uwanja wa Stampford Bridge.

Juan Mata alipachika bao la kwanza la Chelsea kabla ya Frank Lampard kufunga bao la pili kupitia kwaju wa penalti.

Kipa wa Arsenal alimuangusha Ramires ndani ya kijisanduki na kumlazimisha refa wa mechi hiyo kutoa adhabu ya penalti na pia kuumpa kipa huyo kadi ya njano.

Mechi hiyo inaendelea sasa.