Powered By Blogger

Sunday, January 6, 2013

JAHAZI KUJIVINJARI TRAVETINE USIKU WA LEO

 Big Daddy Mzee Yussuf.  Mkali wa taarab hapa nchini Mzee Yussuf leo amepania kukonga nyoyo za mashabiki wake katika show yake ya kwanza kuifanya tangu mwaka huu wa 2013 ulipoingia katika ukumbi wa Travetine Hoteli.

Nguli huyo ambaye natamba na wimbo unaokwenda hewani kwa jina la Wasiwasi wako atawaongoza waimbaji wengine wa kundi hilo kulishambulia jukwaa kuanzia saa tatu usiku mpaka riamba.

 Malkia Leila Rashid anaye atakuepo kwenye onyesho hilo bab kubwa kabisha tangu kuanza kwa mwaka huu.

 Mwasiti naye ataimba

 Mohammed Ali 'Mtoto Pori' ataimba kibao chake kipya kinachofahamika kama 'Kazi mnayo'

 Timu yote hii itakuepo na kila mmoja ataimba kwa raha zake kabisa hivyo mashabiki na wapenzui wote munatakiwa kuhudhuria onyesho hilo la aina yake.

 Mfalme Mzee Yussuf akiimba na wacheza kiduku wake
 Fatma Ali

 Sauti ya Chiriku Hadija Yussuf.

 Rahma Machupa akitunzwa na shabiki wake.

 Mwasiti Kitoronto.

 Mzee Yussuf akiimba.

 Kutoka kushoto ni Leila Rashid, Fatma Kasimu na Kidawa.

 Wazee wa kazi wakiwa kwenye pozi ni Chid Boy na Amigo

 Hao ni Mwasiti na na Rahma Machupa

 Nogesha baba nogesha.

 Mashabiki wa Jahazi wakitibwirika

 Baba Warida Mussa Bezi
 Mzee Yussuf akicheza kidugu

 Warembo wa Jahazi wakiwa kazini
 Ni kiduku kwenda mbele tu
Mzee Yussuf akiimba kwa hisa.

Wakali wa taarabu hapa nchini Jahazi leo watafanya onyesho lao la kwanza tangu kuingia kwa mwaka huu katika ukumbi wao wa nyumbani wa Travetine Hoteli kuanzia saa tatu usiku mpaka riamba.

Kiongozi wa Jahazi Mzee Yussuf amesema onyesho hilo bab kubwa litatakuwa maalumu kwa wapenzi na mashabiki wao na kwamba wataimba nyimbo zao zote mpya na na zile zinazoendelea kuwika kwenye viunga mbalimbali vya burudani.

Amewaomba mashabiki na wapenzi wao kujitokeza kwa wingi ili kupata burudani ya kutosha na kuridhisha katika onyesho hilo.